This is default featured post 1 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured post 2 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured post 3 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured post 4 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured post 5 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
Tuesday, 27 October 2015
MBATIA AMLAZA CHALI MZEE ELYIATONGA MREMA JIMBO LA VUNJO
MAWAZIRI WA JK WLIOANGUKA KWENYE NAFASI YA UBUNGE MWAKA HUU 2015

Wednesday, 21 October 2015
mkuu wa majeshi ya ulinzi nchini Jenerali davis mwamunyange aonekana
![]() |
| Jenerali Davis Mwamunyange |
Alisema hakuna nchi inayoweza kupata maendeleo mbalimbali kama haina jeshi imara kutokana na kuwapo vitendea kazi vya kutosha na madhubuti vinavyoimarisha jeshi hilo.
Jenerali Mwamunyange alisema katika kipindi chote cha uongozi wa Rais Kikwete, ameimarisha JWTZ na kutimiza mahitaji ya jeshi hilo.
Alisema pamoja na changamoto ndogo zilizobaki, lakini anaamini serikali ijayo itazifanyia kazi na kuendeleza pale alipoishia ili kuwa na jeshi imara.
Tuesday, 20 October 2015
zikiwa zimebaki siku 5 kuelekea uchaguzi mkuu, huyu hapa kigogo mwingine wa ccm kutimkia ukawa
![]() |
| Dkt. Eve Sinare akihojiwa na Waandishi wa Habari |
Wimbi la kujivua uanachama lazidi kuitafuna CCM, mwanachama mwingine muhimu aliyefanikisha mipango ya Ushindi wa Rais Jakaya Kikwete kuingia madarakani amehama CCM na kujiunga UKAWA.
Zikiwa zimebaki siku 5 kabla ya Oktoba 25, siku ambayo watanzania wataandika historia ya kuiweka madarakani serikali mpya ya awamu ya Tano, kada mwingine Mkongwe wa Chama hicho, ametangaza rasmi kujiweka kando.
JK akumbushwa kutangaza mali alizochuma kabla ya kung'atuka.
![]() |
| Rais wa Tanzania |
“Rais Kikwete alijaza fomu ya mali alizokuwa nazo Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, lakini hakutangaza. Tunasubiri kuona sasa baada ya kumaliza atatangaza mali aliyopata akiwa madarakani,” alisema.
Alisema mwaka 1995, Rais mstaafu, Benjamin Mkapa, alipoingia madarakani alitangaza mali zake, lakini alipong’atuka, ‘alisahau’ kutangaza, pengine ni kutokana na majukumu aliyokuwa nayo kitaifa sasa tunasubiri kuona kwa Rais Kikwete,” alisema.
Kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma namba 13, 1995 na kanuni zake, mwananchi anaweza kupata taarifa za mali za viongozi kwa kufuata utaratibu uliopo, lakini baada ya kupata taarifa hizo, haruhusiwi kuzitangaza au kuzichapisha kwenye vyombo vya habari.
Chanzo TUBONGE TZ
Chadema yamshtaki Kikwete UN.
![]() |
| Rais wa Tanzania |
Mwanasheria wa Chadema, John Mallya, aliwaeleza waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kuwa barua hiyo waliituma UN jana.
Mallya alisema lengo la barua ni kumshtaki Rais Kikwete kwa mataifa mengine kutokana na kauli yake ya kuwatisha Watanzania aliyodai aliitoa Oktoba 14, mwaka huu ya kuwataka wapigakura kuondoka kituoni baada ya kupiga kura na endapo watakiuka watashughulikiwa.
Mallya alisema kauli ya Rais Kikwete ni kinyume cha Sheria ya Uchaguzi inayomtaka mpigakura kukaa mita 200 kutoka kituo cha kupigia kura.
“Kwa sababu Rais Kikwete hatuwezi kumshtaki kwa mujibu wa sheria za nchi yetu, ziko mamlaka ambazo tunatumia kumshtaki kama tulivyofanya kuiandikia barua UN na kupeleka nakala Jumuiya ya Madola, Umoja wa Afrika, Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai na kusainiwa na Makamu Mwenyekiti wa Chadema, Profesa Abdallah Safari,” alisema Mallya.
Chanzo... TUBONGE TZ
Daktari bandia awaambukiza Ukimwi watu 100
Mwanaume mmoja aliyejidai kuwa daktari na kuwaambukiza watu zaidi ya mia moja virusi amefikishwa mahakamani nchini Cambodia. Yamkini daktari huyo bandia alikuwa akiwadunga wagonjwa wake kwa sindano aliyokuwa ameitumia kwa mgonjwa aliyekuwa na virusi vya Ukimwi.
Yem Chhrin anakabiliwa na kosa la kuua na kuambukiza watu ugonjwa huo kwa kukusudia. Aidha Bw Yem anashtakiwa kwa kuwalaghai watu kuwa ni daktari ilhali hana vyeti halali vya kuhudumia umma. Iwapo atapatikana na hatia mahakama ya nchi hiyo huenda ikamhukumu kifungo cha maisha jela.
Waathiriwa walioambukizwa maradhi ya Ukimwi wanatokea katika kijiji cha Roka kilichoko Kaskazini Magharibi. Mmoja wao ni kiongozi wa kidini wa madhehebu ya Buddha na mtoto wa miaka mitatu.
Takriban 10 kati ya waathiriwa hao wanakisiwa kuwa wameshakata roho. Kwa mujibu wa ripoti za mahakama daktari huyo bandia amekiri kuhudumu bila vyeti maalum ila anakana kukusudia kuwaambukiza watu hao 100 virusi vinavyosababisha maradhi ya Ukimwi.













